Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Jiji La Arusha Juni, 2025
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa za kujaza nafasi za ajira mpya kufuatia kibali cha ajira Kumb. Na. FA/97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili 2025 kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
1.0 DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 15
1.1 Majukumu ya Kazi
-
Kukagua gari kabla na baada ya safari.
-
Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi.
-
Kufanya matengenezo madogo ya gari.
-
Kukusanya na kusambaza nyaraka.
-
Kutunza taarifa za safari kwenye daftari la safari.
-
Kufanya usafi wa gari.
-
Kufanya kazi nyingine kwa maelekezo ya msimamizi.
1.2 Sifa za Mwombaji
-
Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV).
-
Leseni ya Daraja E au C; awe ameendesha kwa mwaka mmoja bila kusababisha ajali.
-
Cheti cha mafunzo ya msingi ya Udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.
1.3 Mshahara
-
Ngazi ya mshahara TGS B1.
2.0 Masharti ya Jumla kwa Waombaji
-
Waombaji wawe raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
-
Kuambatisha cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na mwanasheria au wakili.
-
Kuambatisha Curriculum Vitae yenye mawasiliano na wadhamini 3.
-
Kuambatisha vyeti vya taaluma na elimu vilivyothibitishwa.
-
Testimonial, Provisional Results, Statement of Results na Result Slips hazitakubaliwa.
-
Vyeti vya waliosoma nje vihakikiwe na TCU, NECTA au NACTE.
-
Waliofukuzwa au kustaafishwa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali.
-
Waajiriwa wa Umma walioko kwenye nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba.
-
Wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba na waeleze aina ya ulemavu kwenye mfumo.
-
Wenye tofauti ya majina waambatanishe DEED POLL.
-
Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.
-
Waombaji walioteuliwa kwa usaili wanashauriwa kuvaa mavazi yanayozuia baridi kutokana na hali ya hewa ya Arusha.
-
Mwisho wa kutuma maombi: 25 Juni 2025.
-
Barua ya maombi iandikwe kwa:
Mkurugenzi,
Halmashauri ya Jiji la Arusha,
S.L.P 3013, 20 Barabara ya Boma, 23101 ARUSHA.
-
Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya mtandao kupitia: https://portal.ajira.go.tz
Imetolewa na:
Dr. Nindwa Maduhu
KAIMU MKURUGENZI WA JIJI – HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA
Makala Nyingine: