Walimu Walioitwa Kazini 2025/2026 Kupitia Ajira Portal

Filed in Ajira, Uncategorized by on May 23, 2025 23 Comments

Majina ya Walimu Walioitwa Kazini 2025/2026 Kupitia Ajira Portal  (orodha na list ya majina kwenye PDF walioajiriwa 2025 na vituo vyao vya kazi) Majina ya walimu waliopata kazi 2025 MAJINAYA WALIOITWA KAZINI WALIMU KADA ZA UALIMU.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kati ya tarehe 14-08-2024 na tarehe 17-01-2025 kuwa matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili.

Orodha ya majina haya pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana.

Majina ya Walimu Walioitwa Kazini 2025

Waombaji waliofaulu usaili wanatakiwa kuchukua barua za kupangiwa kituo cha kazi katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma zilizopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwenye Majengo ya Dkt. Asha Rose Migiro, Masjala ya wazi ndani ya siku saba kutoka tarehe ya tangazo hili na baada ya hapo barua ambazo hazitachukuliwa na wahusika zitatumwa kupitia anuani zao za Posta.

Aidha, waombaji kazi waliofaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua za kupangiwa kituo cha kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya kupewa barua ya Ajira.

Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite
kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa.

MUHIMU:

Wanaokuja kuchukua barua za kupangiwa kituo cha kazi wanapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi; Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:-

  • Kitambulisho cha Uraia,
  • Hati ya kusafiria,
  • Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi,
  • Kitambulisho cha Mpiga kura au
  • Leseni ya Udereva.

Orodha Ya Majina Kamili:

https://www.ajira.go.tz/

Tags: ,

About the Author ()

Comments (23)

Trackback URL | Comments RSS Feed

  1. Neema Joseph says:

    Mimi jamani mbona sijapangwa na nilihitimi chuo 2016??Nisaidieni na Mimi mtoto wa mkulima hata mlo mmija ni shida.

  2. jires nzingo says:

    ulisoma masomo yapi?

  3. Hope says:

    Mbona ualimu daraja la IIIA, hayaonekani?

  4. Riziki Yahya says:

    Idadi mbona ni ndogo sana? Au zinatoka kwa awamu?

    Pia, walimu waliokuwemo kwenye database ni wenye sifa zipi? Wamefaulu written na oral interview au ni wa miaka ya nyumba?

  5. Milka says:

    Serikali tunaomba na sisi watu wa pharmacy mtusaidie tumekaa sana mtaani ht mitaji hatuna na tunategemewa mtukumbuke na sisi halo ni mbaya sana

  6. Milka says:

    Serikali tunaomba na sisi watu wa pharmacy hasa sisi pharm tech mtaani kugumu sana na familia zinatutegemea na mitaji ni changamoto mtupe nasi ajira tunaomba.

  7. Winnie albert says:

    Aisee mbna mnatoa majina kidogokidogo sana ,toeni majina mengi ili mtu ajue kuwa apepangwa au hajapangwa afanye mambo mengine .

  8. Winnie says:

    Aisee mbna mnatoa majina kidogokidogo sana ,toeni majina mengi ili mtu ajue kuwa apepangwa au hajapangwa afanye mambo mengine .

  9. Anna TILA says:

    Naomba na mm basi ata jina langu liandikwe uko maan daah naumia kuona Majin ya wengine TU

    • Veronica nyamtumbaga says:

      Maisha ni magumu mtaani serikal tunaomba mtuangalie kwa jicho la pili miaka nane mtaani had vyeti vinazeeka duuh

  10. Jmn serikal naomb waendelee kutoa majna ya Elimu ya Awali maan cna amani kabis familia inanitegemea na cna cha kufany naomb sana😭

  11. GETRUDANSIA bonifasi kihunrwa says:

    Jamani naombeni na mm Mungu awatangulie mtume na jina langu kwani mtaani ni pagimu jamani narudia kuangali mara tatutatu Wala jina silioni jamani tusaidieni

  12. Dastan says:

    walimu wa elimu ya awali mashulen hamna hadi wanachukuliwa walimu kazin waende semina kujifunza kufundisha elimu ya awali wakati sisi mmetuzalisha wengi lakin mnatuaacha mtaani mnachukua 20 tunaomba mtufikirie jamn🙏

  13. James Thomas Getana says:

    Samahan jaman naomba bas mtuajiri walimu tunaojitolea .. mfano mm nimejitolea huu ni mwaka wa tano nipo bado najitolea

  14. Tunaomba muahiri walimu tuliofanyia njombe interview jaman

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.