Tetesi Za Usajili Simba 2025/2026 Leo, Klabu ya Simba SC, maarufu kama Wekundu wa Msimbazi, inachora ramani mpya kuelekea msimu wa 2025/2026, baada ya msimu uliopita wa mafanikio na changamoto.
Kutinga nusu fainali ya Kombe la Shirikisho CAF na kumaliza ligi ya NBC kwa tofauti ya pointi moja nyuma ya Yanga, kumewasha moto wa mabadiliko ya ndani kwa ndani.
Vuguvugu La Usajili: Safari Mpya Ya Simba SC Yaendelea
Karibu Simba SC, Alassane Kante (@a_m_kante80).
Kwa taarifa zaidi tumia Simba App, Simba Mastori (piga 0900010000) au Instagram Subscriptions. #NguvuMoja
Karibu Simba SC, Rushine De Reuck. (@rushine23_rd3)
Kwa taarifa zaidi tumia Simba App, Simba Mastori au Instagram Subscriptions. #NguvuMoja
Simba imeingia sokoni mapema kwa nia ya kuimarisha kikosi, baada ya kikao kizito cha Bodi ya Wakurugenzi kilichoongozwa na MO Dewji na kupokea ripoti ya kocha Fadlu Davids. Ripoti hiyo imeibua maeneo sita nyeti ya kuimarishwa—kutoka safu ya ulinzi hadi ushambuliaji, lengo kuu likiwa ni kurejesha hadhi ya Simba kitaifa na kimataifa.
- Mshambuliaji wa kati – mwenye uwezo zaidi ya Mukwala na Ateba.
- Beki wa kati – mwenye uzoefu na uthabiti wa CAF.
- Kiungo mkabaji – mbadala bora wa Ngoma/Kagoma.
- Kiungo namba 10 – mwenye uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi.
- Winga wa kulia – mwenye kasi na mbinu zaidi ya Mutale.
- Mshambuliaji msaidizi – kusaidia mzigo wa Ahoua.
Majina Yaliyo Katika Hatua za Mwisho za Mikataba
Mchezaji | Nafasi | Hali ya Mkataba |
---|---|---|
Aishi Manula | Kipa | Kuondoka rasmi |
Shomari Kapombe | Beki wa kulia | Sintofahamu |
Mohammed ‘Tshabalala’ | Beki wa kushoto | Hajaongezewa mkataba |
Fabrice Ngoma | Kiungo | Anaweza kuondoka |
Usajili Unaotembelea Mlangoni Msimbazi
1. Ismaila Kante (CA Bizertin – Senegal)
Kiungo mwenye nguvu, mbunifu na mwenye uzoefu Tunisia, anatarajiwa kutua Msimbazi kwa ada ya Dola 285,000. Anatarajiwa kuungana na Kagoma kuimarisha safu ya ulinzi wa katikati.
2. Rodrigue Kossi (Benin)
Kiungo huru baada ya kuachana na ES Sétif ya Algeria. Ana nafasi kubwa ya kujiunga kutokana na hali yake ya kuwa mchezaji huru sokoni.
3. Charve Onoya (Union Maniema – DR Congo)
Kiungo mshambuliaji mwenye kasi na uwezo wa kupenya ngome za wapinzani. Anatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa Ahoua.
Vilio na Vicheko: Wanaotajwa Kuondoka au Kurudi
Walio Kwenye Dirisha la Kutoka:
- Mukwala – anaweza kuuzwa kwa klabu ya Afrika Kaskazini.
- Ngoma – hajathibitisha kubaki.
- Tshabalala – atachukuliwa na timu nyingine ikiwa Simba haitafanya haraka.
Walio Katika Mipango ya Kurudi:
- Sadio Kanoute – licha ya kuondoka, ameripotiwa kuwemo kwenye mipango ya kurejeshwa.
- Clatous Chama – baada ya changamoto Yanga, kuna fununu za kurejea Msimbazi.
Nafasi | Mchezaji Anaehusishwa | Chanzo cha Usajili |
---|---|---|
Beki wa kati | Abdallah Klandana | Fountain Gate |
Beki wa pembeni | Karim | JKT Tanzania |
Kipa mpya | Yakubu Suleiman | Taarifa za ndani |
Kiungo mkabaji | Iginho Epalanga (Angola) | Karibu kutangazwa |
Yatakayoboreshwa Kwa Kipaumbele:
- Kipa wa kiwango cha CAF – atakayeleta ushindani kwa Camara.
- Kiungo wa kati mwenye ‘box-to-box power’
- Mshambuliaji matata wa kufunga mechi kubwa
- Mabingwa wa kasi pembeni (wingers)
Hitimisho: Simba Haichezi na Usajili Safari Hii
Msimu wa 2025/2026 unakaribia, na Simba SC tayari imeonesha dhamira ya kweli ya kufanya mageuzi makubwa. Kwa mikakati ya mapema, usajili unaoelekezwa na ripoti ya kitaalamu, na dhamira ya MO Dewji, Wekundu wa Msimbazi wanajiandaa kurejea kwenye kilele cha soka la Afrika Mashariki.
Ratiba ya Mechi za Simba Ligi Kuu Ya NBC 2024/2025 Tanzania
Simba Yatangaza haitocheza Mechi Ya Derby Tar 8, Machi 2025
mubadala wa ahoa yupo aliye saini