Ratiba ya ligi kuu NBC Tanzania 2024/25 Bara

Ratiba ya ligi kuu NBC Tanzania 2024/25 Bara, msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025 Unaojulikana ka  (NBC Premier league) Unaendelea kwa kishindo msimu huu wa 2024/2025. 

Ligi Kuu ya Tanzania Bara maarufu kama NBC Premier League 2024/2025 imeshika kasi huku timu 16 zikishiriki katika mbio kali za kutwaa taji la ubingwa. Msimu huu, unaoanza mnamo Agosti 16, 2024, unatarajiwa kuwa wa kipekee kutokana na ushindani wa juu na uimarishaji wa vikosi vya timu nyingi maarufu.

Kutoka kwa mabingwa watetezi Yanga SC hadi kwa wageni kama Pamba Jiji FC na Kengold FC, mashabiki wanatarajia kuona burudani ya hali ya juu.

Ratiba ya ligi kuu NBC Tanzania 2024/25 Bara 

 

Ratiba ya Mzunguko wa Ligi Kuu 2024/2025

Kipindi cha kwanza cha ligi, kinachojumuisha mzunguko wa 1 hadi 30, kitaanza kwa kishindo na kumalizika mnamo Mei 24, 2025. Hapa chini ni ratiba kamili:

Mzunguko Tarehe Mechi
1 Agosti 16, 2024 Pamba Jiji vs Tanzania Prisons
2 Agosti 24, 2024
3 Septemba 11, 2024
4 Septemba 14, 2024
5 Septemba 21, 2024
6 Septemba 28, 2024
7 Oktoba 2, 2024
8 Oktoba 19, 2024 Simba SC vs Yanga SC
9 Oktoba 26, 2024
10 Novemba 2, 2024
11 Novemba 9, 2024
12 Novemba 23, 2024
13 Novemba 30, 2024
14 Desemba 11, 2024
15 Desemba 14, 2024
16 Desemba 21, 2024
17 Desemba 28, 2024
18 Januari 18, 2025
19 Januari 25, 2025
20 Februari 1, 2025
21 Februari 15, 2025
22 Februari 22, 2025
23 Machi 1, 2025
24 Machi 8, 2025
25 Machi 29, 2025
26 Aprili 12, 2025
27 Aprili 19, 2025
28 Mei 3, 2025
29 Mei 17, 2025
30 Mei 24, 2025

Mechi Zinazotarajiwa kwa Hamasa

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Simba SC na Yanga SC watakutana mnamo Oktoba 19, 2024, katika moja ya mechi zinazovuta hisia zaidi nchini. Pia, pazia la msimu wa 2024/2025 litafungwa kwa mechi nane kwa wakati mmoja mnamo Mei 24, 2025.

Timu Zenye Mtazamo wa Ushindi

Yanga SC, mabingwa watetezi, wanafanya kila juhudi kutetea taji lao huku Simba SC nao wakiwa na kiu ya kulipiza kisasi na kutwaa ubingwa baada ya kupoteza msimu uliopita. Timu kama Azam FC na Geita Gold pia zimeimarisha vikosi vyao ili kujiweka sawa kwa ajili ya ushindani wa ubingwa.

Pamba Jiji FC na Kengold FC, timu mpya zilizopanda daraja, zitakuwa na mtihani mzito wa kuonyesha uwezo wao katika ngazi ya juu. Mashabiki wanatarajia kuona kama timu hizi mpya zitaweza kufurukuta dhidi ya majabali ya soka la Tanzania.

Ligi Daraja la Kwanza (Championship)

Wakati Ligi Kuu ya NBC inaendelea, mechi za Ligi Daraja la Kwanza zitaanza mnamo Septemba 14, 2024, na kumalizika mnamo Mei 10, 2025. Ligi hii pia imekuwa kivutio kikubwa kwa timu zinazopigania kupanda daraja na kuingia kwenye Ligi Kuu.

Fainali ya Kombe la FA

Kombe la FA, moja ya mashindano maarufu nchini, linaendelea kuvutia hisia za mashabiki wengi. Fainali ya kombe hili imeratibiwa kufanyika Mei 31, 2025. Timu zote kubwa za Ligi Kuu zitaingia uwanjani kutafuta nafasi ya kutwaa taji hili la heshima.

Msimu wa NBC Premier League 2024/2025 unaahidi kuwa wa kusisimua na wenye ushindani mkubwa. Huku mashabiki wakiwa na shauku ya kuona timu zao zikifanya vizuri, watarajie burudani ya hali ya juu kila wikiendi.

Makala Nyingine: