Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Ngorongoro Juni, 2025
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa stahiki kujaza nafasi za ajira mpya kufuatia kibali cha ajira Kumb. Na. FA.97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili 2025 kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
1.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4
1.1 Sifa za Mwombaji
-
Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) au Kidato cha Sita (Form VI).
-
Stashahada (Diploma) au NTA Level 6 katika fani ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
-
Awe na ujuzi wa kompyuta.
1.2 Majukumu ya Kazi
-
Kuorodhesha barua zinazoingia na zinazotoka.
-
Kusambaza na kurudisha majalada kwa watendaji.
-
Kutafuta na kurudisha nyaraka katika sehemu husika.
-
Kufuatilia mzunguko wa majalada (File Tracking).
1.3 Mshahara
-
Ngazi ya mshahara TGS C1.
2.0 DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 4
2.1 Sifa za Mwombaji
-
Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV).
-
Leseni ya Daraja E au C, awe ameendesha kwa muda usiopungua mwaka mmoja bila kusababisha ajali.
-
Cheti cha mafunzo ya msingi ya Udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.
2.2 Majukumu ya Kazi
-
Kukagua gari kabla na baada ya safari.
-
Kuwapeleka watumishi katika safari za kikazi.
-
Kufanya matengenezo madogo ya gari.
-
Kukusanya na kusambaza nyaraka.
-
Kutunza taarifa za safari katika daftari la safari.
-
Kufanya usafi wa gari.
2.3 Mshahara
-
Ngazi ya mshahara TGS B1.
3.0 MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 5
3.1 Sifa za Mwombaji
-
Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV).
-
Stashahada (Diploma) au NTA Level 6 ya Uhazili.
-
Kuwa amefaulu somo la Hatimkato (Shorthand) ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja.
-
Awe na ujuzi wa Programu za Ofisi za Kompyuta (Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail, Publisher).
3.2 Majukumu ya Kazi
-
Kuchapa barua, taarifa na nyaraka mbalimbali.
-
Kupokea wageni na kuwahudumia.
-
Kutunza kumbukumbu za matukio, miadi, safari, na ratiba za vikao.
-
Kutafuta na kusambaza majalada kwa maofisa husika.
-
Kupanga dondoo na kuandaa vikao mbalimbali.
-
Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.
3.3 Mshahara
-
Ngazi ya mshahara TGS C1.
4.0 Masharti ya Jumla kwa Waombaji
-
Waombaji wawe raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
-
Wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba na kueleza aina ya ulemavu kwenye mfumo.
-
Kuambatisha Curriculum Vitae yenye maelezo ya mawasiliano na wadhamini 3.
-
Kuambatisha vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na mwanasheria au wakili.
-
Testimonial, Provisional Results, Statement of Results na Result Slips hazitakubaliwa.
-
Vyeti vya waliosoma nje vihakikiwe na TCU, NECTA au NACTE.
-
Waliofukuzwa au kustaafishwa katika utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali.
-
Waajiriwa wa Umma walioko kwenye nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba.
-
Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.
-
Waombaji wa nafasi za Dereva II waambatishe vyeti vya mafunzo ya Udereva.
-
Majina yanayofautiana yaambatane na DEED POLL.
-
Mwisho wa kutuma maombi: 29 Juni 2025.
-
Barua ya maombi iandikwe kwa:
MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA NGORONGORO
S.L.P 1, LOLIONDO
-
Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya mtandao kupitia: https://portal.ajira.go.tz
Imetolewa na:
Murtallah S. Mbillu
MKURUGENZI MTENDAJI, HALMASHAURI YA WILAYA YA NGORONGORO
.pdf TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA NGORONGORO 16-06-2025
Makala Nyingine: