Timu zilizofuzu Makundi Kombe La Shirikisho Africa 2025/2026 CAF, Kwenye makala hii tutaona orodha ya Timu zilizofuzu hatua ya makundi CAFCL Kombe La Shirikisho Africa.
Ni rasmi sasa! Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) limetangaza majina ya vilabu 16 vilivyofanikiwa kufuzu hatua ya makundi ya CAF Confederation Cup 2025/26.

Mashindano haya yanatarajiwa kuwa moto wa kuotea mbali, yakihusisha vigogo wa zamani pamoja na sura mpya zenye kiu ya mafanikio makubwa.
Orodha ya Timu 16 Zilizofuzu Hatua ya Makundi
| Na. | Timu | Nchi |
|---|---|---|
| 1 | Azam FC | Tanzania |
| 2 | Singida Black Stars | Tanzania |
| 3 | Zamalek SC | Misri |
| 4 | CR Belouizdad | Algeria |
| 5 | Wydad AC | Morocco |
| 6 | Maniema Union | DRC Congo |
| 7 | Zesco United | Zambia |
| 8 | USM Alger | Algeria |
| 9 | FC San Pedro | Ivory Coast |
| 10 | OC Safi | Morocco |
| 11 | Kaizer Chiefs | Afrika Kusini |
| 12 | Stellenbosch FC | Afrika Kusini |
| 13 | AS Otohô | Congo Brazzaville |
| 14 | Djoliba AC | Mali |
| 15 | Nairobi United | Kenya |
| 16 | Al Masry SC | Misri |
🇹🇿 Fahari ya Tanzania
Tanzania imeandika historia kwa mara nyingine, baada ya Azam FC na Singida Black Stars kuingia hatua ya makundi kwa kishindo kikubwa.
Mashabiki wa soka nchini wamefurahia mafanikio haya, wakiamini kuwa mwaka huu huenda nchi hiyo ikatoa bingwa mpya wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Vigogo wa Afrika Waja Kivingine
Vilabu vikongwe kama Zamalek SC, Wydad AC, na USM Alger vinakuja na uzoefu mkubwa wa michuano ya kimataifa, vikiahidi kufanya mashindano haya kuwa ya kusisimua zaidi.
Kwa upande mwingine, timu kama Stellenbosch na Nairobi United zinawakilisha kizazi kipya cha vilabu vinavyopanda kwa kasi barani Afrika.
Matarajio
Hatua ya makundi inatarajiwa kuanza Novemba 2025, ambapo timu zitapangwa kwenye makundi manne (A–D), kila moja likiwa na timu nne.
Mashabiki wanatarajia mechi kali, hasa zile zitakazozikutanisha vigogo wa Afrika Mashariki dhidi ya mabingwa wa Kaskazini na Kusini mwa Afrika.
Makala Nyingine:









Tuachie Maoni Yako