Taarifa Kwa Umma kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) yatangaza kuhusiana na taarifa za uongo kuhusu SAMIA SCHOLARSHIP kwa mwaka 2024/2025

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inatoa tahadhari kwa wanafunzi na wananchi wote kuhusu taarifa potofu zinazozunguka kwenye mitandao ya kijamii na makundi ya ‘WhatsApp’ kuhusu sifa za kuomba, maeneo ya ufadhili, na tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ya SAMIA SCHOLARSHIP kwa mwaka 2024/2025.

Kwa mujibu wa Bodi ya Mikopo, taarifa hizi siyo za kweli na zinapaswa kupuuzwa mara moja. HESLB inasisitiza kuwa mwongozo rasmi na sahihi kuhusiana na ufadhili huu wa SAMIA SCHOLARSHIP unapatikana kupitia tovuti yake rasmi: www.heslb.go.tz pamoja na kurasa za mitandao ya kijamii zinazotambulika kwa jina la HESLB Tanzania.

Tahadhari Kuhusu Taarifa Potofu

Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na taarifa zisizo na ukweli zinazosambazwa kwenye majukwaa mbalimbali ya kidijitali kuhusu mchakato wa kuomba SAMIA SCHOLARSHIP. Baadhi ya taarifa hizo zinadai kuwa bado kuna muda wa kuomba au kutoa sifa zisizokubalika kwa wanafunzi walengwa.

HESLB inapinga vikali taarifa hizo na inawakumbusha wananchi kuwa chanzo pekee cha taarifa za kuaminika kuhusu programu hii ni kupitia vyanzo rasmi vilivyotajwa hapo juu.

Tovuti na Mitandao Rasmi ya HESLB

HESLB imeweka wazi kuwa taarifa zote muhimu zinazohusiana na ufadhili wa SAMIA SCHOLARSHIP kwa mwaka 2024/2025 zimekuwa zikipatikana kwenye tovuti yake na kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii. Hivyo, wanafunzi na wananchi wanaaswa kufuatilia taarifa kupitia njia hizi ili kuepuka kupotoshwa na taarifa zisizo rasmi.

Tovuti ya HESLB:

Makala Nyingine: