Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu Mei, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu anawatangazia Watanzania wote wenye sifa kutuma maombi ya ajira kwa nafasi zilizoidhinishwa kupitia kibali cha ajira mpya kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kama ifuatavyo:

1. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 5

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Kidato cha Sita (VI).
  • Leseni ya Daraja “C” au “E”.
  • Uzoefu wa kuendesha magari kwa mwaka 1 bila kusababisha ajali.
  • Cheti cha mafunzo ya uendeshaji kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari.
  • Kuwasafirisha watumishi.
  • Matengenezo madogo ya gari.
  • Kusambaza nyaraka na kutunza logbook.
  • Kufanya usafi wa gari na kazi nyingine kwa maelekezo ya msimamizi.

Mshahara:

  • Ngazi ya Mshahara: TGS B

2. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 6

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
  • Stashahada ya Uhazili (NTA Level 6).
  • Uwezo wa Hatimkato Kiswahili na Kiingereza (maneno 100 kwa dakika).
  • Ujuzi wa programu za kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, Publisher.

Majukumu:

  • Kuchapa nyaraka na barua za kawaida na siri.
  • Kupokea wageni na kuwasiliana kuhusu mahitaji yao.
  • Kutunza ratiba, kumbukumbu na majalada.
  • Kusaidia maandalizi ya vikao na vifaa vya ofisi.

Mshahara:

  • Ngazi ya Mshahara: TGS C

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI:

  • Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri kati ya miaka 18 – 45 (isipokuwa waajiriwa wa Serikali).
  • Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kuainisha aina ya ulemavu wao kwenye mfumo wa maombi.
  • Aambatishe CV, anuani, namba za simu, barua pepe, na majina ya wadhamini watatu wa kuaminika.
  • Vyeti vya elimu na taaluma vihalalishwe na Mwanasheria/Wakili.
  • “Statement of results”, “Provisional Results”, “Results Slips” hazikubaliki.
  • Waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU, NECTA au NACTE.
  • Wastaafu wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  • Waajiriwa katika nafasi za kuingilia hawapaswi kuomba.
  • Maombi ya sifa au taarifa za kughushi yatapelekea hatua za kisheria.

MAELEKEZO YA UOMBANJI:

Maombi yaambatane na barua ya maombi iliyosainiwa na vyeti vyote vya elimu.

Barua ielekezwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji

Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
S.L.P. 50,
USHETU – KAHAMA

Maombi yatumwe kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ajira: https://portal.ajira.go.tz

Mwisho wa kutuma maombi: 09 Juni 2025

Imetolewa na:

Hadija M. Kabojela
Mkurugenzi Mtendaji (W)
Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.