Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Songea Mei, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea amepokea kibali cha ajira kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Hivyo, anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:

1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 05

Majukumu:

  • Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na siri.
  • Kupokea na kuelekeza wageni.
  • Kutunza kumbukumbu za matukio, vikao na safari za mkuu wake.
  • Kupokea na kusambaza majalada.
  • Kuandaa vifaa vya ofisi na maandalizi ya vikao.
  • Kutekeleza kazi nyingine utakazopangiwa na mkuu wa kazi.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV).
  • Diploma ya Uhazili au cheti cha NTA Level 6 ya Uhazili.
  • Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza (maneno 80 kwa dakika).
  • Ujuzi wa programu za ofisi (Word, Excel, PowerPoint, Email, Internet, Publisher).

Ngazi ya Mshahara: TGS C1

2. Dereva Daraja la II – Nafasi 03

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari.
  • Kuwapeleka watumishi safarini.
  • Kufanya matengenezo madogo ya gari.
  • Kusambaza nyaraka.
  • Kuweka kumbukumbu za safari na kufanya usafi wa gari.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne au Sita.
  • Leseni ya Daraja C au E yenye uzoefu wa mwaka 1 bila ajali.
  • Mafunzo ya msingi ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Ngazi ya Mshahara: TGS B1

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

  • Raia wa Tanzania, umri miaka 18 hadi 45.
  • Ambatanisha CV yenye anwani, simu, barua pepe na referees 3 wa kuaminika.
  • Watumishi wa umma waambatanishe barua kupitia kwa waajiri wao.
  • Vyeti vyote vya elimu na taaluma viwe vimehakikiwa na Mwanasheria/Wakili.
  • Hati za matokeo (Statement of Results), Provisional na Testmonials HAZITAKUBALIWA.
  • Waliosoma nje wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NECTA/NACTE.
  • Waliostaafu hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  • Taarifa/sifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.

Mwisho wa kutuma maombi: 10 Juni, 2025.

JINSI YA KUTUMA MAOMBI:

Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa Ajira Portal: https://portal.ajira.go.tz

Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

Anwani ya barua:

Mkurugenzi Mtendaji (W)
Halmashauri ya Wilaya ya Songea
Barabara ya Halmashauri
S. L. P 995
57183, SONGEA – RUVUMA

Imetolewa na:

Elizabeth M. Gumbo
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.