Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida anawatangazia Watanzania wote wenye sifa kuomba nafasi za ajira zilizoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 kama ifuatavyo:
1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 5
Sifa za Mwombaji:
- Awe amefaulu Kidato cha Nne (IV) au Kidato cha Sita (VI).
- Awe na Stashahada (Diploma) au NTA Level 6 ya Uhazili.
- Awe amefaulu somo la Hatimkato kwa Kiswahili na Kiingereza maneno 100 kwa dakika.
- Awe na ujuzi wa programu za kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Email, Internet na Publisher.
Majukumu:
- Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na za siri.
- Kupokea wageni na kuelekeza huduma.
- Kutunza kumbukumbu na ratiba za Mkuu wake.
- Kusaidia maandalizi ya vikao na orodha ya vifaa.
Mshahara:
-
Ngazi ya Serikali: TGS C.
2. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 3
Sifa za Mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne (IV).
- Leseni ya daraja “C” au “E” na uzoefu wa kuendesha bila ajali angalau mwaka 1.
- Cheti cha Mafunzo ya Uendeshaji kutoka VETA au chuo kinachotambulika na Serikali.
Majukumu:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari.
- Kuwasafirisha watumishi na nyaraka.
- Kuweka rekodi za safari (logbook) na kufanya usafi wa gari.
- Kufanya matengenezo madogo na kazi nyingine zitakazoelekezwa.
Mshahara:
-
Ngazi ya Serikali: TGS B.
MASHARTI YA JUMLA:
- Awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45.
- Aambatishe nakala ya cheti cha kuzaliwa.
- Awe na wasifu binafsi (CV) ulio kamili na picha mbili za “passport size”.
- Aambatishe vyeti halisi vya taaluma vinavyotambulika na Serikali.
- “Statement of Results” na “Provisional Results” hazikubaliki.
Waliomaliza masomo nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na NECTA, NACTE au TCU.
- Wastaafu hawaruhusiwi kuomba bila kibali maalum.
- Waajiriwa wa Serikali waliopo katika nafasi za kuingilia hawapaswi kuomba.
MAELEKEZO YA UOMBANJI:
Barua ya maombi ielekezwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Singida
S.L.P. 27, SINGIDA
Maombi yote yawasilishwe kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ajira:
👉 https://portal.ajira.go.tz
Mwisho wa kutuma maombi: 10 Juni 2025
Imetolewa na:
Ester Chaula
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Singida