Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Nyang’hwale Mei, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale amepokea kibali cha ajira mpya kutoka kwa Katibu Mkuu – Utumishi kwa ajili ya mwaka wa fedha 2024/2025. Hivyo, anakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:

1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 04

Majukumu:

  • Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na siri.
  • Kupokea na kuelekeza wageni.
  • Kutunza kumbukumbu za matukio, miadi, vikao na safari za mkuu wake.
  • Kupokea na kusambaza majalada kwa maofisa husika.
  • Kuandaa mahitaji ya vifaa vya ofisi na maandalizi ya vikao.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha Nne au Sita.
  • Diploma ya Uhazili au cheti cha NTA Level 6.
  • Uwezo wa hati mkato wa Kiswahili na Kiingereza (maneno 100 kwa dakika).
  • Ujuzi wa programu za ofisi kama Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, na Publisher.

Ngazi ya Mshahara: TGS C

2. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 02

Majukumu:

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka kwenye rejista.
  • Kusambaza na kurudisha majalada kwa watendaji.
  • Kuchambua, kupanga na kuhifadhi nyaraka kulingana na somo husika.
  • Kutunza mafaili kwenye masijala.
  • Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha Nne au Sita.
  • Diploma ya Masijala (NTA Level 6) kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
  • Ujuzi wa kutumia kompyuta.

Ngazi ya Mshahara: TGS C

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

  • Awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45 (isipokuwa walioko Serikalini).
  • Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kuainisha aina ya ulemavu kwenye mfumo.
  • Ambatanisha CV, anwani, barua pepe, simu, na majina ya wadhamini 3.
  • Ambatanisha vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na Wakili.
  • “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of Results” HAZITAKUBALIWA.
  • Waliosoma nje wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NECTA/NACTVET.
  • Wastaafu wa umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  • Watumishi wa umma walioko katika nafasi za kuingilia wasitume maombi.
  • Sifa au taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 12 Juni, 2025.

MUHIMU:
Barua ya maombi iliyosainiwa ielekezwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya,
S.L.P 352,
NYANG’HWALE

Namna ya Kutuma Maombi:

Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa Ajira Portal: https://portal.ajira.go.tz

Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA NYANG’HWALE

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.