Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara amepokea kibali cha ajira kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa ajili ya utekelezaji wa ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Hivyo, anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:
1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 4
Majukumu:
- Kuchapa barua, taarifa na nyaraka mbalimbali.
- Kupokea na kuelekeza wageni.
- Kutafuta na kuhifadhi majalada na nyaraka.
- Kuandaa dondoo na maandalizi ya vikao.
- Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya kidato cha nne au sita.
- Stashahada (Diploma) ya Uhazili au NTA Level 6 ya Uhazili.
- Uwezo wa hatimkato Kiswahili na Kiingereza (maneno 100 kwa dakika).
- Ujuzi wa kompyuta (Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, Publisher).
Mshahara: Ngazi ya Serikali TGS C1
2. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4
Majukumu:
- Kurekodi barua zinazoingia na kutoka.
- Kusambaza na kurudisha majalada.
- Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya kidato cha nne au sita.
- Cheti cha stashahada (NTA Level 6) katika fani ya utunzaji kumbukumbu.
- Ujuzi wa kompyuta.
Mshahara: Ngazi ya Serikali TGS C1
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
- Kuambatisha cheti cha kuzaliwa.
- Kuwasilisha wasifu binafsi (CV) unaojitosheleza.
- Kuambatisha vyeti vya taaluma, kidato cha nne/sita (sio “provisional” au “statement of results”).
- Kuambatisha picha mbili (passport size) za hivi karibuni.
- Waliosoma nje wahakikishe vyeti vyao vimethibitishwa na NECTA/NACTE/TCU.
- Wastaafu wa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali.
- Waajiriwa wa serikali walioko katika nafasi za kuingilia wasitume maombi.
- Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.
- Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 12 Juni, 2025.
JINSI YA KUTUMA MAOMBI:
Barua ya maombi ielekezwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
S.L.P 30, NGARA
Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya Ajira Portal kupitia: https://portal.ajira.go.tz
Maombi yasiyotumwa kupitia mfumo wa Ajira Portal HAYATAFANYIWA KAZI.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
 Simu: 028 2226016 |  Barua pepe: [email protected]
Tovuti: www.ngaradc.go.tz