Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Mwanga 02-06-2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za ajira baada ya kupokea kibali kutoka kwa Katibu Mkuu – Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kumb. Na. FA.228/613/01G/085 ya tarehe 12 Mei, 2025.
1. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 7
Majukumu ya Kazi:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari
- Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi
- Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari
- Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali
- Kutunza taarifa za safari (logbook)
- Kufanya usafi wa gari
- Kazi nyingine kadri atakavyoelekezwa
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV)
- Leseni ya Daraja E au C yenye uzoefu wa mwaka 1 bila kusababisha ajali
- Cheti cha Mafunzo ya Udereva (Basic Driving Course) kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali
Ngazi ya Mshahara:
Serikali – TGS B
MASHARTI YA JUMLA:
- Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri usiozidi miaka 45 (isipokuwa walioko kazini serikalini)
- Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na waeleze aina ya ulemavu kwenye mfumo
- Ambatanisha cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili
- Watumishi wa Umma waliopata sifa mpya wapitishe maombi kwa waajiri wao
- Ambatanisha CV yenye taarifa kamili, namba za mawasiliano na wadhamini 3
- Ambatanisha vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili
- “Testimonial,” “Provisional Results,” “Statement of Results” na result slips HAZITAKUBALIWA
- Waliomaliza masomo nje ya Tanzania wawasilishe vyeti vilivyohakikiwa na TCU, NECTA au NACTE
- Wastaafu wa umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi
- Watumishi walioko kwenye nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba
- Wanaowasilisha taarifa za uongo watachukuliwa hatua za kisheria
- Mwisho wa kutuma maombi: 17 Juni, 2025
Maombi Yatumwe Kwa:
MKURUGENZI MTENDAJI (W),
HALMASHAURI YA WILAYA YA MWANGA,
S.L.P. 176, MWANGA
+255 26 2757652
+255 26 2756463
[email protected]
www.mwangadc.go.tz
Njia ya Kutuma Maombi:
Wasilisha maombi kupitia mfumo wa kielektroniki wa Ajira: https://portal.ajira.go.tz
Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu HAYATAZINGATIWA.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA MWANGA
Makala Nyingine: