Mkurugenzi wa Mji Nanyamba anawatangazia Watanzania wote wenye sifa kuomba ajira kufuatia kibali cha ajira mpya kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa nafasi zifuatazo:
1. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 8
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
- Leseni ya Daraja “E” au “C” na uzoefu usiopungua mwaka 1 bila kusababisha ajali.
- Cheti cha Mafunzo ya Msingi ya Ufundi Stadi (VETA) au kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
Majukumu:
- Kukagua gari kabla/baada ya safari.
- Kuwapeleka watumishi kazini.
- Kufanya matengenezo madogo.
- Kusambaza nyaraka, kutunza logbook na kufanya usafi wa gari.
- Kufanya kazi zingine utakazopangiwa na msimamizi.
Mshahara:
- Ngazi ya Mshahara: TGS B1.
2. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 9
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
- Diploma au NTA Level 6 ya Uhazili.
- Ufundi wa Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza (maneno 80 kwa dakika).
- Ujuzi wa programu za kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Email, Internet, Publisher.
Majukumu:
- Kuchapa nyaraka.
- Kupokea na kuelekeza wageni.
- Kutunza kumbukumbu, ratiba, na majalada.
- Kuandaa vifaa vya ofisi na kusaidia vikao.
Mshahara:
- Ngazi ya Mshahara: TGS C1.
3. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 5
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
- Diploma (NTA level 6) katika fani ya Masjala kutoka chuo kinachotambulika na Serikali.
- Ujuzi wa Kompyuta.
Majukumu:
- Kuorodhesha barua zinazoingia/kutoka.
- Kusambaza na kurudisha majalada.
- Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.
Mshahara:
- Ngazi ya Mshahara: TGS C1.
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI:
- Awe raia wa Tanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
- Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba na kutaja aina ya ulemavu wao.
- Aambatishe CV, anuani, namba ya simu, barua pepe na majina ya wadhamini 3.
- Vyeti vya elimu na taaluma vihalalishwe na mwanasheria.
- “Statement of Results”, “Provisional Results”, “Results Slips” havikubaliki.
- Waombaji waliomaliza nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na NECTA, NACTE, au TCU.
- Wastaafu wa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali maalum.
- Maombi yasiyo zingatia masharti haya hayatapokelewa.
MAELEKEZO YA UOMBANJI:
Maombi yaambatane na barua ya maombi iliyosainiwa na vyeti husika.
Barua ielekezwe kwa:
Mkurugenzi wa Mji
Halmashauri ya Mji Nanyamba
S.L.P. 1490,
NANYAMBA – MTWARA
Maombi yatumwe kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ajira:
👉 https://portal.ajira.go.tz
Mwisho wa kutuma maombi: 09 Juni 2025
Tangazo limetolewa na:
Eng. Mshamu A. Munde
Mkurugenzi wa Mji
Halmashauri ya Mji Nanyamba