Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Madaba 28-05-2025, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba anatangaza nafasi za kazi kwa Watanzania wote wenye sifa stahiki, kufuatia kibali cha ajira kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Kumb. Na. FA.97/288/01/A/25 ya tarehe 25/04/2025).
Kumb. Na. MDC/CL.10/7/56 | Tarehe: 28 Mei, 2025
1.0 MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 2
Sifa za Mwombaji:
- Kuajiriwa mwenye Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV);
- Awe na Stashahada (Diploma) ya Uhazili au NTA Level 6;
- Uwezo wa kuchapa Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika;
- Mafunzo ya programu za kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email na Publisher.
Majukumu:
- Kuchapa nyaraka mbalimbali;
- Kupokea na kuelekeza wageni;
- Kutunza ratiba, kumbukumbu na miadi ya Mkuu wake;
- Kupanga dondoo za vikao na kutunza mahitaji ya ofisi;
- Kufanya kazi nyingine zitakazopangwa na Mkuu wa Idara.
Mshahara: TGS C1
2.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 7
Sifa za Mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI);
- Stashahada au NTA Level 6 ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali;
- Ujuzi wa kompyuta.
Majukumu:
- Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka;
- Kusambaza na kurudisha majalada kwa watendaji;
- Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.
Mshahara: TGS C1
3.0 DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 5
Sifa za Mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV);
- Leseni ya Daraja C au E;
- Uzoefu wa mwaka mmoja bila kusababisha ajali;
- Cheti cha Mafunzo ya Udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.
Majukumu:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari;
- Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi;
- Kutunza daftari la safari, kufanya usafi wa gari na matengenezo madogomadogo;
- Kusambaza nyaraka.
Mshahara: TGS B1
4.0 MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Mwombaji awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45;
- Ambatanisha CV yenye maelezo ya kina, anuani ya barua, namba za simu, email, na wadhamini watatu;
- Ambatanisha vyeti vya elimu vilivyothibitishwa na wakili: cheti cha kidato cha IV/VI, diploma, computer na kitaaluma;
- HAKUBALIKI: Testmonial, Provisional results, Statement of results, Result slips;
- Vyeti vya nje ya nchi vihakikiwe na TCU/NACTE/NECTA;
- Wastaafu hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi;
- Waliopo kazini waombe kwa kupitia waajiri wao;
- Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria;
- Mwisho wa kutuma maombi: 09 Juni, 2025.
5.0 JINSI YA KUTUMA MAOMBI
- Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa ajira (Recruitment Portal):
👉 https://portal.ajira.go.tz - Barua za maombi ziandikwe kwa anuani ifuatayo:
Mkurugenzi Mtendaji (W),
Halmashauri ya Wilaya ya Madaba,
38 Barabara ya Kifaguro Magingo,
S.L.P. 10, 57186 – MADABA, SONGEA.
Imetolewa na:
SAJIDU I. MOHAMED
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA
- Tangazo La Nafasi Za Kazi – Halmashauri Ya Wilaya Ya Mlele (Mei 2025)
- Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Mvomero Mei, 2025
- Majina Ya Walioitwa Kazini Utumishi Na Ajira Portal 2025
- Nafasi za Kazi Jeshi la Zimamoto 2025/2026 Tangazo la ajira zimamoto 2025 pdf
- TANGAZO LA KUITWA KAZINI Tarehe: 24 Aprili 2025 Taasisi Mbalimbali za Umma