Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Hai 02-06-2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai anatangaza nafasi za kazi kwa Watanzania wenye sifa na ujuzi, kufuatia kibali cha ajira kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Kumb. Na. FA.97/228/01/A/25 ya tarehe 29 Aprili, 2025).
1. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 11
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV)
- Leseni ya Daraja E au C yenye uzoefu wa mwaka 1 bila kusababisha ajali
- Mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na serikali
Majukumu ya Kazi:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari
- Kuwapeleka watumishi safarini
- Kutunza logbook na kufanya usafi wa gari
- Kukusanya na kusambaza nyaraka
Mshahara:
Ngazi ya Serikali – TGS B
2. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 5
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne au Sita
- Diploma/Stashahada ya Uhazili (NTA Level 6)
- Uwezo wa kuandika Hatimkato (maneno 100 kwa dakika, Kiswahili & Kiingereza)
- Ujuzi wa Kompyuta: Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, Publisher
Majukumu ya Kazi:
- Kuchapa nyaraka
- Kupokea na kuelekeza wageni
- Kutunza ratiba, kumbukumbu na nyaraka
- Kuwasiliana na kusaidia Mkuu wa Idara
Mshahara:
Ngazi ya Serikali – TGS C
3. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne/Sita
- Diploma (NTA Level 6) ya Masijala kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali
Majukumu ya Kazi:
- Kupanga na kuhifadhi nyaraka
- Kutafuta kumbukumbu zinazohitajika
- Kuweka nyaraka kwenye mafaili
- Kushughulikia maombi ya kumbukumbu
Mshahara:
Ngazi ya Serikali – TGS C
4. MHUDUMU WA JIKONI DARAJA LA II – NAFASI 1
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne
- Cheti cha mafunzo ya uhudumu wa jikoni kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali
Majukumu ya Kazi:
- Kusafisha vyombo na maeneo ya chakula
- Kusaidia wapishi
- Kuweka vifaa vya mezani
Mshahara:
Ngazi ya Serikali – TGOS A
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45
- Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kueleza aina ya ulemavu
- Ambatanisha CV yenye maelezo kamili, mawasiliano na wadhamini 3
- Vyeti vya “Result Slip”, “Provisional”, “Statement of Results” havitakubaliwa
- Vyeti vyote vya elimu na taaluma vihakikiwe na Mwanasheria/Wakili
- Waliosoma nje ya nchi wawasilishe uthibitisho kutoka NECTA, NACTE au TCU
- Wastaafu wa Serikali hawaruhusiwi kuomba bila kibali maalum
- Watumishi wa Umma walioko kwenye nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba
- Wanaowasilisha taarifa za kughushi watachukuliwa hatua za kisheria
- Mwisho wa kutuma maombi: 15 Juni, 2025
Barua ya maombi ielekezwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya Hai
3BR-TTCL-Kanisani, S.L.P. 27, Bomang’ombe – HAI, KILIMANJARO
Maombi yawasilishwe kwa njia ya mtandao kupitia: https://portal.ajira.go.tz
Maombi nje ya utaratibu huu hayatazingatiwa.
TANGAZO LIMETOLEWA NA:
MKURUGENZI MTENDAJI –
HALMASHAURI YA WILAYA YA HAI
Makala Nyingine: