Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze June, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze anatangaza nafasi za kazi kwa Watanzania wenye sifa, kufuatia kibali kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Kumb. Na. FA.97/228/01/A/25 ya tarehe 29 Aprili, 2025).

1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI (5)

Majukumu ya Kazi:

  • Kuchapa barua, nyaraka za kawaida na za siri
  • Kupokea na kuelekeza wageni
  • Kutunza ratiba na kumbukumbu za vikao
  • Kusimamia majalada na nyaraka
  • Kuandaa mahitaji ya vifaa vya ofisi
  • Kazi nyingine atakayopangiwa na mkuu wake

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne au Sita
  • Stashahada (NTA Level 6) ya Uhazili
  • Uwezo wa kuandika kwa Hatimkato maneno 100 kwa dakika moja (Kiswahili na Kiingereza)
  • Ujuzi wa Kompyuta katika programu za Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, na Publisher

Mshahara:

Kwa mujibu wa viwango vya Serikali – TGS C

2. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI (4)

Majukumu ya Kazi:

  • Kuwasafirisha watumishi kwa safari za kikazi
  • Kusambaza nyaraka
  • Kutunza log-book
  • Kufanya matengenezo madogomadogo ya gari
  • Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne au Sita
  • Leseni ya Daraja C au E yenye uzoefu wa mwaka 1
  • Mafunzo ya msingi ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali

Mshahara:

Kwa mujibu wa viwango vya Serikali – TGS B

MASHARTI YA JUMLA:

  • Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45
  • Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kueleza aina ya ulemavu
  • Ambatanisha CV yenye maelezo kamili, namba ya simu, barua pepe na wadhamini 3
  • Vyeti vya “Result Slip,” “Provisional,” “Testimonials” havitakubaliwa
  • Cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili
  • Wastaafu wa Serikali hawaruhusiwi kuomba bila kibali maalum
  • Watumishi wa Umma walioko katika nafasi za kuingilia wasitume maombi
  • Vyeti vyote vya taaluma viwe vimehakikiwa na Mwanasheria/Wakili
  • Waliosoma nje ya nchi wawasilishe uthibitisho kutoka TCU, NECTA, au NACTE
  • Wanaowasilisha taarifa za uongo watachukuliwa hatua za kisheria
  • Barua ya maombi iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza
  • Mwisho wa kutuma maombi: 15 Juni, 2025

Maombi yote yawasilishwe kwa anuani:
MKURUGENZI MTENDAJI (W), HALMASHAURI YA WILAYA YA CHALINZE, S.L.P 65, CHALINZE.

Maombi yatumiwe kupitia mfumo wa kielektroniki wa Ajira kupitia:
👉 https://portal.ajira.go.tz

Maombi nje ya utaratibu huu hayatazingatiwa.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHALINZE

TANGAZO LA AJIRA CHALINZE.pdf

Makala Nyingine:

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.