Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Biharamulo Mei, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo amepokea kibali cha utekelezaji wa ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Hivyo anakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:

1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 05

Majukumu ya Kazi:

  • Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na siri.
  • Kupokea na kusaidia wageni.
  • Kutunza ratiba na kumbukumbu za mkuu wake.
  • Kuandaa vikao na mahitaji ya ofisi.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
  • Diploma au NTA Level 6 ya Uhazili.
  • Uwezo wa hati mkato maneno 100 kwa dakika kwa Kiswahili na Kiingereza.
  • Ujuzi wa programu za kompyuta (Word, Excel, PowerPoint, Email, Publisher).

Ngazi ya Mshahara: TGS C

2. Dereva Daraja la II – Nafasi 06

Majukumu ya Kazi:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari.
  • Kuwapeleka watumishi safarini.
  • Kufanya usafi na matengenezo madogo ya gari.
  • Kutunza kumbukumbu za safari.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha Nne.
  • Leseni ya Daraja C au E.
  • Uzoefu wa mwaka 1 bila ajali.
  • Mafunzo ya msingi ya udereva kutoka VETA, NIT au chuo kinachotambulika.

Ngazi ya Mshahara: TGS B

3. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 04

Majukumu ya Kazi:

  • Kutafuta, kupanga na kuhifadhi kumbukumbu.
  • Kuweka nyaraka kwenye majalada na reki.
  • Kuhudumia maombi ya kumbukumbu kutoka taasisi mbalimbali.

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya kidato cha Nne au Sita.
  • Diploma (NTA Level 6) ya Utunzaji wa Kumbukumbu katika fani za Afya, Masjala, Mahakama au Ardhi.

Ngazi ya Mshahara: TGS C

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

  • Awe raia wa Tanzania, umri miaka 18–45 (isipokuwa walioko serikalini).
  • Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kutaja aina ya ulemavu kwenye mfumo.
  • Ambatanisha cheti cha kuzaliwa na nakala ya kitambulisho cha NIDA.
  • Ambatanisha CV, vyeti vya taaluma, kidato cha nne/sita na mafunzo ya kazi.
  • Ambatanisha picha moja ya passport size (iandikwe jina nyuma).
  • “Statement of Results” hazitakubaliwa.
  • Waliosoma nje wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NACTE/NECTA.
  • Waajiriwa wa Serikali walioko kwenye nafasi za kuingilia wasitume maombi.
  • Maelezo ya kughushi yatapelekea hatua za kisheria.
  • Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 06 Juni, 2025.

MUHIMU:

Barua ya maombi iliyosainiwa ielekezwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya,
S.L.P 70,
BIHARAMULO

Namna ya Kutuma Maombi:

Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa Ajira (Recruitment Portal) kwa kutumia kiunganishi: https://portal.ajira.go.tz

Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatazingatiwa.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI WA WILAYA
HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.