Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo amepokea kibali cha utekelezaji wa ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Hivyo anakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:
1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 05
Majukumu ya Kazi:
- Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na siri.
- Kupokea na kusaidia wageni.
- Kutunza ratiba na kumbukumbu za mkuu wake.
- Kuandaa vikao na mahitaji ya ofisi.
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
- Diploma au NTA Level 6 ya Uhazili.
- Uwezo wa hati mkato maneno 100 kwa dakika kwa Kiswahili na Kiingereza.
- Ujuzi wa programu za kompyuta (Word, Excel, PowerPoint, Email, Publisher).
Ngazi ya Mshahara: TGS C
2. Dereva Daraja la II – Nafasi 06
Majukumu ya Kazi:
- Kukagua gari kabla/baada ya safari.
- Kuwapeleka watumishi safarini.
- Kufanya usafi na matengenezo madogo ya gari.
- Kutunza kumbukumbu za safari.
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya kidato cha Nne.
- Leseni ya Daraja C au E.
- Uzoefu wa mwaka 1 bila ajali.
- Mafunzo ya msingi ya udereva kutoka VETA, NIT au chuo kinachotambulika.
Ngazi ya Mshahara: TGS B
3. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 04
Majukumu ya Kazi:
- Kutafuta, kupanga na kuhifadhi kumbukumbu.
- Kuweka nyaraka kwenye majalada na reki.
- Kuhudumia maombi ya kumbukumbu kutoka taasisi mbalimbali.
Sifa za Mwombaji:
- Elimu ya kidato cha Nne au Sita.
- Diploma (NTA Level 6) ya Utunzaji wa Kumbukumbu katika fani za Afya, Masjala, Mahakama au Ardhi.
Ngazi ya Mshahara: TGS C
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Awe raia wa Tanzania, umri miaka 18–45 (isipokuwa walioko serikalini).
- Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kutaja aina ya ulemavu kwenye mfumo.
- Ambatanisha cheti cha kuzaliwa na nakala ya kitambulisho cha NIDA.
- Ambatanisha CV, vyeti vya taaluma, kidato cha nne/sita na mafunzo ya kazi.
- Ambatanisha picha moja ya passport size (iandikwe jina nyuma).
- “Statement of Results” hazitakubaliwa.
- Waliosoma nje wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NACTE/NECTA.
- Waajiriwa wa Serikali walioko kwenye nafasi za kuingilia wasitume maombi.
- Maelezo ya kughushi yatapelekea hatua za kisheria.
- Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 06 Juni, 2025.
MUHIMU:
Barua ya maombi iliyosainiwa ielekezwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya,
S.L.P 70,
BIHARAMULO
Namna ya Kutuma Maombi:
Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa Ajira (Recruitment Portal) kwa kutumia kiunganishi: https://portal.ajira.go.tz
Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatazingatiwa.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI WA WILAYA
HALMASHAURI YA WILAYA YA BIHARAMULO