Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Mbozi june, 2025
Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Mbozi 08-06-2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kwamba, baada ya kupata kibali cha ajira kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Utumishi wa Umma, anakaribisha maombi ya kazi kwa nafasi zifuatazo:
1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 5
Majukumu:
- Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na za siri
- Kupokea wageni na kuwapa msaada
- Kutunza kumbukumbu za miadi na ratiba
- Kuandaa mahitaji ya vifaa vya ofisi n.k.
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne au Sita
- Stashahada ya Uhazili (NTA Level 6)
- Ufahamu wa Hatimkato (maneno 100 kwa dakika) kwa Kiswahili na Kiingereza
- Ujuzi wa programu za kompyuta za ofisi
Mshahara: TGS C
2. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4
Majukumu:
- Kusajili barua zinazoingia na kutoka
- Kusambaza majalada kwa watendaji
- Kutunza na kufuatilia mzunguko wa majalada n.k.
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne au Sita
- Stashahada ya Utunzaji Kumbukumbu (NTA Level 6)
- Ujuzi wa kompyuta
Mshahara: TGS C
3. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 7
Majukumu:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari
- Kuwapeleka watumishi kazini
- Kutunza taarifa za safari n.k.
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne
- Leseni ya Daraja E au C yenye uzoefu wa mwaka 1
- Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali
Mshahara: TGS B1
MASHARTI YA JUMLA:
- Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45.
- Wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na kueleza aina ya ulemavu wao.
- Ambatanisha:
- CV ya kina
- Vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na wakili/mwanasheria
- Majina ya wadhamini watatu (referees)
- HAKUBALIKI:
- Provisional results, statement of results, au slips za matokeo ya kidato cha nne/sita
- Waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU, NECTA au NACTVET.
- Waliostaafu bila kibali hawaruhusiwi kuomba.
- Ajira hii si kwa waajiriwa walioko kwenye nafasi za kuingilia katika Utumishi wa Umma.
- Maombi ya uongo yatapelekea hatua za kisheria.
- Majina tofauti kwenye vyeti yawasilishwe na hati ya kiapo (deed poll).
- Mwisho wa kutuma maombi: 21 Juni 2025
JINSI YA KUTUMA MAOMBI:
- Maombi yaambatane na barua ya maombi iliyoandikwa na kusainiwa, pamoja na vyeti husika.
- Anwani ya barua:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi
S.L.P 3
Mbozi
Tuma maombi kupitia mfumo wa kielektroniki: https://portal.ajira.go.tz/
Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA YA MBOZI
Makala Nyingine:
Tags: Nafasi Za Kazi, Wilaya Mbozi