Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Mbozi june, 2025

Filed in Ajira by on June 9, 2025 0 Comments

Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Mbozi 08-06-2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kwamba, baada ya kupata kibali cha ajira kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Utumishi wa Umma, anakaribisha maombi ya kazi kwa nafasi zifuatazo:

1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 5

Majukumu:

  • Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na za siri
  • Kupokea wageni na kuwapa msaada
  • Kutunza kumbukumbu za miadi na ratiba
  • Kuandaa mahitaji ya vifaa vya ofisi n.k.

Sifa za Mwombaji:

  • Kidato cha Nne au Sita
  • Stashahada ya Uhazili (NTA Level 6)
  • Ufahamu wa Hatimkato (maneno 100 kwa dakika) kwa Kiswahili na Kiingereza
  • Ujuzi wa programu za kompyuta za ofisi

Mshahara: TGS C

2. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 4

Majukumu:

  • Kusajili barua zinazoingia na kutoka
  • Kusambaza majalada kwa watendaji
  • Kutunza na kufuatilia mzunguko wa majalada n.k.

Sifa za Mwombaji:

  • Kidato cha Nne au Sita
  • Stashahada ya Utunzaji Kumbukumbu (NTA Level 6)
  • Ujuzi wa kompyuta

Mshahara: TGS C

3. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 7

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari
  • Kuwapeleka watumishi kazini
  • Kutunza taarifa za safari n.k.

Sifa za Mwombaji:

  • Kidato cha Nne
  • Leseni ya Daraja E au C yenye uzoefu wa mwaka 1
  • Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali

Mshahara: TGS B1

MASHARTI YA JUMLA:

  • Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45.
  • Wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na kueleza aina ya ulemavu wao.
  • Ambatanisha:
    • CV ya kina
    • Vyeti vya elimu na taaluma vilivyothibitishwa na wakili/mwanasheria
    • Majina ya wadhamini watatu (referees)
    • HAKUBALIKI:
  • Provisional results, statement of results, au slips za matokeo ya kidato cha nne/sita
  • Waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU, NECTA au NACTVET.
  • Waliostaafu bila kibali hawaruhusiwi kuomba.
  • Ajira hii si kwa waajiriwa walioko kwenye nafasi za kuingilia katika Utumishi wa Umma.
  • Maombi ya uongo yatapelekea hatua za kisheria.
  • Majina tofauti kwenye vyeti yawasilishwe na hati ya kiapo (deed poll).
  • Mwisho wa kutuma maombi: 21 Juni 2025

JINSI YA KUTUMA MAOMBI:

  • Maombi yaambatane na barua ya maombi iliyoandikwa na kusainiwa, pamoja na vyeti husika.
  • Anwani ya barua:

Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi
S.L.P 3
Mbozi

Tuma maombi kupitia mfumo wa kielektroniki: https://portal.ajira.go.tz/

Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA YA MBOZI

Makala Nyingine:

Tags: ,

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.