Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Manispaa Ya Sumbawanga 27-05-2025, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga anatangaza nafasi za ajira kwa Watanzania wote wenye sifa stahiki kujaza nafasi kumi na moja (11) zilizotokana na kibali kutoka kwa Katibu Mkuu – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
1.0 NAFASI ZINAZOTANGAZWA
1.1 Dereva Daraja la II – Nafasi 8
Majukumu ni pamoja na:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari;
- Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi;
- Kufanya matengenezo madogo ya gari;
- Kusambaza nyaraka mbalimbali;
- Kujaza taarifa za safari katika daftari;
- Kufanya usafi wa gari na kazi nyingine zitakazopangiwa na mwajiri.
Sifa za mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV);
- Leseni ya daraja E au C;
- Uzoefu wa kuendesha gari kwa mwaka mmoja bila kusababisha ajali;
- Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.
Ngazi ya mshahara: TGS B
1.2 Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 3
Majukumu ni pamoja na:
- Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka kwenye Rejista;
- Kusambaza na kupokea majalada kwa watendaji;
- Kutafuta na kurudisha nyaraka/majalada sehemu husika;
- Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya taasisi.
Sifa za mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne au Sita;
- Stashahada/Diploma (NTA Level 6) ya Utunzaji Kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali;
- Ujuzi wa kutumia kompyuta.
Ngazi ya mshahara: TGS C
2.0 MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Mwombaji awe raia wa Tanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
- Waombaji wenye ulemavu wanahimizwa kutuma maombi na waeleze aina ya ulemavu waliokuwa nao kwenye mfumo.
- Ambatanisha:
- CV yenye maelezo ya kutosha,
- Anuani ya barua, namba ya simu, barua pepe,
- Majina ya wadhamini watatu wa kuaminika.
- Ambatanisha pia vyeti halisi vilivyothibitishwa na Mwanasheria au Wakili:
- Cheti cha kidato cha nne au sita,
- Cheti cha taaluma (Diploma, Cheti, Degree),
- Vyeti vya kitaaluma na kompyuta.
- Hati za matokeo (Result slips, Provisional results, Statement of results) hazitakubaliwa.
- Waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na kuthibitishwa na TCU, NECTA au NACTE.
- Waliostaafu hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
- Wanaotuma taarifa za kughushi watachukuliwa hatua za kisheria.
- Mwisho wa kutuma maombi: 03 Juni, 2025.
3.0 NAMNA YA KUTUMA MAOMBI
Barua ya maombi iwe imeandikwa na kusainiwa, ikiambatana na vyeti vyote muhimu. Anuani ya barua ielekezwe kwa:
Mkurugenzi wa Manispaa
Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga
S.L.P. 187
Maombi yote yawasilishwe kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal):
👉 https://portal.ajira.go.tz
Maombi yote yatakayowasilishwa nje ya utaratibu huu hayatafanyiwa kazi.
Imetolewa na:
Mangali U. E
Mkurugenzi wa Manispaa – Sumbawanga
Makala Nyingine: