Ajira

Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Manispaa ya Shinyanga Mei, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga amepokea kibali cha ajira mpya kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:

1. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 04

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au Sita (Form VI).
  • Diploma au NTA Level 6 katika fani ya utunzaji kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
  • Ujuzi wa kutumia kompyuta.

Majukumu:

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka kwenye rejista.
  • Kusambaza na kupokea majalada kutoka kwa watendaji.
  • Kufuatilia mzunguko wa majalada (file tracking).
  • Kupanga, kuchambua na kuhifadhi nyaraka kwa mujibu wa somo husika.
  • Kuhudumia watafiti na kurudisha majalada kwenye ghala.

Ngazi ya Mshahara: TGS C1 (Ajira ya kudumu)

2. Dereva Daraja la II – Nafasi 10

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au Sita (Form VI).
  • Leseni ya Daraja C au E.
  • Uzoefu wa mwaka mmoja bila kusababisha ajali.
  • Mafunzo ya msingi ya udereva kutoka VETA, NIT au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari.
  • Kuwapeleka watumishi safarini.
  • Kufanya matengenezo madogo, usafi na kuandika taarifa za safari kwenye daftari.
  • Kukusanya na kusambaza nyaraka.

Ngazi ya Mshahara: TGS B1 (Ajira ya kudumu)

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

  • Raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45 (isipokuwa walioko Serikalini).
  • CV ya kina yenye anwani, simu, na referees watatu wa kuaminika.
  • Ambatanisha vyeti vya elimu (Kidato cha Nne/Sita), taaluma na cheti cha kuzaliwa.
  • “Result Slip”, “Statement of Results”, “Provisional Results” HAZITAKUBALIWA.
  • Waliomaliza masomo nje ya nchi wawasilishe uthibitisho kutoka NECTA au TCU.
  • Maombi yawasilishwe kwa Kiswahili au Kiingereza.
  • Waombaji wenye ulemavu waeleze mahitaji yao kwenye barua ya maombi.
  • Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria.
  • Waliostaafu hawaruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

Mwisho wa kutuma maombi: tarehe 13 Juni, 2025.

Namna ya Kutuma Maombi:

Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa Ajira Portal: https://portal.ajira.go.tz

Maombi yatakayowasilishwa nje ya mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

Anwani ya barua:

Mkurugenzi wa Manispaa
Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa
Barabara ya Mwanza, Chamaguha
S.L.P. 28, Shinyanga
Simu: 028-2763213
Barua pepe: [email protected]
Tovuti: www.shinyangamc.go.tz

TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA SHINYANGA .pdf

Imetolewa na:

Mwl. Alexius R. Kagunze
MKURUGENZI WA MANISPAA – SHINYANGA

Leave a Comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.