Tangazo La Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Manispaa Ya Shinyanga 01-06-2025, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa, kufuatia kibali cha ajira mpya kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia barua yenye Kumb. Na. FA.97/288/01/A/25 ya tarehe 29 Aprili, 2025.
Zifuatazo ni nafasi za kazi zilizotangazwa:
1. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI (4)
Sifa za Mwombaji:
- Cheti cha Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI)
- Stashahada/NTA level 6 ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali
- Ujuzi wa Kompyuta
Majukumu ya Kazi:
- Kuorodhesha barua zinazoingia/zinazotoka
- Kusambaza na kufuatilia majalada
- Kupanga nyaraka kulingana na masomo husika
- Kuhifadhi kumbukumbu na kusaidia watafiti
Masharti ya Ajira:
- Ajira ya kudumu, Mshahara kwa mujibu wa ngazi ya TGS C1
2. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI (10)
Sifa za Mwombaji:
- Kidato cha Nne au Sita
- Leseni ya Daraja la C au E yenye uzoefu wa mwaka 1 bila ajali
- Mafunzo ya uendeshaji magari kutoka VETA/NIT au Chuo kinachotambuliwa na Serikali
Majukumu ya Kazi:
- Ukaguzi na usafi wa gari
- Kuwasafirisha watumishi
- Kutunza taarifa za safari na nyaraka
Masharti ya Ajira:
- Ajira ya kudumu, Mshahara kwa mujibu wa ngazi ya TGS B1
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45 (isipokuwa waliopo kazini Serikalini)
- Awe na CV yenye taarifa kamili, anuani, namba ya simu na wadhamini 3 wa kuaminika
- Aambatishe nakala za vyeti vya elimu (Kidato cha Nne/Sita, Taaluma, Kuzaliwa) – Result Slip, Statement of Results, Provisional Results au Transcripts hazitakubaliwa
- Waliomaliza masomo nje ya nchi wawasilishe uthibitisho wa NECTA (kwa O/A-Level) au TCU (kwa vyuo)
- Barua ya maombi isainiwe na mwombaji, ieleweke kwa Kiswahili au Kiingereza
- Wenye ulemavu waonyeshe mahitaji yao maalum
- Waombaji waliowahi kuajiriwa Serikalini na kuacha kwa sababu yoyote wasijitokeze isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi
- Mwisho wa kutuma maombi: 13 Juni, 2025
Maombi yatumwe kupitia mfumo wa ajira mtandaoni (Recruitment Portal): 👉 https://portal.ajira.go.tz
(Kupitia tovuti ya Sekretarieti ya Ajira, sehemu ya ‘Recruitment Portal’)
Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu huu hayatazingatiwa
Imetolewa na:
Mwl. Alexius R. Kagunze
MKURUGENZI WA MANISPAA YA SHINYANGA
 www.shinyangamc.go.tz
 [email protected] |  028-2763213
TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA SHINYANGA .pdf
Makala Nyingine: