Nafasi Za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Bumbuli

Filed in Ajira by on June 1, 2025 0 Comments

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli amepokea kibali cha ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Hivyo, anakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa kwa nafasi zifuatazo:

1. MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 03

Sifa za Mwombaji:

  • Awe amefaulu Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
  • Awe na Stashahada (Diploma) au Cheti cha NTA level 6 ya Uhazili.
  • Awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza kwa maneno 100 kwa dakika.
  • Awe na ujuzi wa kutumia programu za ofisi kama Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail, na Publisher.

Majukumu:

  • Kuchapa barua na nyaraka za kawaida na za siri.
  • Kupokea wageni na kuelekeza wapi pa kupata huduma.
  • Kutunza kumbukumbu na ratiba za kazi za mkuu wake.
  • Kutafuta na kuratibu majalada/nyaraka.
  • Kuandaa dondoo na vifaa vya mikutano.

Mshahara:

Ngazi ya mshahara wa Serikali – TGS C.

2. DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 05

Sifa za Mwombaji:

  • Awe na Cheti cha Kidato cha Nne (IV).
  • Awe na leseni ya daraja ‘C’.
  • Uzoefu wa kuendesha gari angalau mwaka 1 bila kusababisha ajali.
  • Awe amehitimu mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari.
  • Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi.
  • Kufanya matengenezo madogo ya gari.
  • Kutunza daftari la safari (log book).
  • Kusambaza nyaraka mbalimbali.
  • Kusafisha gari na kazi nyingine kama atakavyoelekezwa.

Mshahara:

Ngazi ya mshahara wa Serikali – TGS B.

3. MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

  • Awe Mtanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45.
  • Awe na cheti cha kuzaliwa.
  • Awasilishe wasifu binafsi (CV) yenye anuani, namba za simu na majina ya wadhamini.
  • Ambatanisha nakala za vyeti vya kitaaluma, kidato cha Nne/Sita na mafunzo mengine.
  • “Statement of Results” au “Provisional Results” hazitakubalika.
  • Ambatanisha picha mbili (passport size) za hivi karibuni.
  • Waliosoma nje wahakikishe vyeti vyao vimeidhinishwa na TCU/NECTA/NACTE.
  • Wastaafu wa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba bila kibali maalum.
  • Waombaji walioko katika utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba kwa nafasi hizi za kuingilia.
  • Wanaotoa taarifa za kughushi watachukuliwa hatua za kisheria.

Mwisho wa kutuma maombi: 09 Juni 2025

4. MAELEKEZO YA KUTUMA MAOMBI:

Barua ya maombi iliyosainiwa iambatishwe na vyeti muhimu na iandikwe kwenda kwa:

Mkurugenzi Mtendaji,

Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli, S.L.P. 111,

BUMBULI.

Njia ya kutuma maombi:

Wasilisha maombi kupitia mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal): https://portal.ajira.go.tz

Imetolewa na:

Baraka M. Zikatimu
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli

Tags: ,

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.