Nafasi za Kazi Zimamoto 2025 ajira Jinsi Ya Kutuma Maombi

Filed in Ajira by on March 15, 2025 5 Comments

Nafasi za Kazi Jeshi la Zimamoto 2025 ajira zimamoto 2025 Jinsi Ya Kutuma Maombi ajira.zimamoto.go.tz Ajira za,Tangazo la ajira zimamoto 2025/2026 pdf Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limetangaza nafasi mpya za ajira kwa vijana wa Kitanzania waliohitimu kidato cha nne na ngazi ya shahada. Nafasi hizo zitatolewa kwa ngazi ya Konstebo kwa wale wanaokidhi vigezo vilivyoainishwa.

Tangazo la ajira zimamoto 2025 pdf

Taarifa hii imetolewa rasmi leo, Alhamisi, Februari 13, 2025, na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, John Masunga. Ingawa idadi ya nafasi za kazi haijawekwa wazi, waombaji wanahimizwa kutuma maombi kabla ya tarehe ya mwisho, Februari 28, Mwaka 2025.

Vigezo vya Kustahiki Ajira

Waombaji wanapaswa kukidhi masharti yafuatayo:

Sifa Maelezo
Uraia Awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa
Umri Miaka 18 – 25 kwa waombaji wa kawaida, 18 – 35 kwa marubani wa helikopta
Urefu Wanaume: Futi 5.7+, Wanawake: Futi 5.4+
Afya Awe na afya njema kimwili na kiakili
Tabia Asiwe na rekodi ya uhalifu, asiwe na tattoo mwilini
Ndoa Asiwe ameoa au kuolewa
Ajira ya awali Asiwe ameajiriwa serikalini hapo awali

Sifa za Ziada kwa Wenye Ujuzi Maalum

Jeshi limeeleza kuwa waombaji wenye taaluma au ujuzi ufuatao wanapewa kipaumbele:

  1. Udereva wa magari makubwa (leseni daraja E, umri miaka 18-28)
  2. Ufundi bomba
  3. Uuguzi
  4. Taaluma ya Zimamoto na Uokoaji
  5. Utabibu
  6. Urubani wa helikopta

Kwa waombaji wenye shahada, fani zinazopendelewa ni:

  • Uhandisi wa bahari na ndege
  • Lugha (Kiingereza)
  • Ukadiriaji majenzi
  • Teknolojia ya habari
  • Uchumi
  • Sheria (waliomaliza shule ya sheria kwa vitendo)
  • Ualimu
  • Usafirishaji barabara na reli
  • Uhandisi wa kemikali

Jinsi ya Kuomba

Waombaji wanapaswa kutuma maombi kupitia mfumo rasmi wa ajira wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji unaopatikana kupitia kiunganishi:

👉 ajira.zimamoto.go.tz

Nyaraka Muhimu za Kuambatisha

  1. Barua ya maombi iliyoandikwa kwa mkono
  2. Nakala ya cheti cha kuzaliwa
  3. Fomu ya uthibitisho wa afya kutoka kwa mganga wa serikali
  4. Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au namba ya NIDA
  5. Picha ya pasipoti ya hivi karibuni
  6. Namba ya mtihani wa kidato cha nne

Waombaji wote wanahimizwa kuzingatia vigezo vyote na kutuma maombi kabla ya tarehe 28 Februari 2025.

Tangazo hili halihusishi malipo yoyote katika mchakato wa kuomba ajira.

Kwa maelezo zaidi, tembelea tovuti rasmi ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji au ofisi zao zilizo karibu nawe.

Soma Makala Nyingine:

Fomu ya Uchunguzi wa Afya (PDF)

Nafasi Za Kazi TRA 2025 Ajira Mpya 1592 Zilizotangazwa

Nafasi za Kazi Kutoka MDAs NA LGAs February 2025

Tags:

About the Author ()

Comments (5)

Trackback URL | Comments RSS Feed

  1. Condrat Mlaponi says:

    Kwa wale ambao wamesomea course ya maendeleo ya jamii wanaweza kupata kipaumbele

  2. Helmina says:

    I face challenge in password when I try to forgot it brought link at mid night when I wake it has expired sorry I need you are help In my password

  3. M says:

    It Look like your web developer stuck in a washing machines

  4. Hussein Bendera says:

    Serikali imetuacha mtaani muda mrefu mpaka leo tunashindwa kuomba nafasi mbalimbali za kazi eti kwa kigezo cha umri, yaani kwakuwa nina umri wa miaka 30 basi siwezi kuajiriwa eti kutokana na umri ni mkubwa

    Sasa katika hili nani alaumiwe, sio kosa langu ila hii wameweka vigezo ambavyo sio sawa tumemaliza vyuo muda mrefu ajira zinatolewa chache tena zinabana wengine, yani hii ndiyo ile mtoto ulimuacha shule bado mdogo wewe umemaliza hadi chuo muda then yeye anakuja kupata ajira kabla yako eti kwa kuwa ana umri sahihi yaani miaka 18 – 28 hili jambo linaongeza sana chuki dhidi ya serikali kwani wanatuambia vigezo ambavyo vinakandamiza wasomi wa muda mrefu ambao wao wenyewe ndiyo wamewakosesha ajira

    INAUMA SANA HILI ILA IPO SIKU TUTAPATA MTETEZI

  5. Hussein Bendera says:

    UBAGUZI WA KI UMRI UMEJITOKEZA

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.