Vifurushi vya Bima ya afya NHIF 2024 (Bei na Gharama Zake)

Vifurushi vya Bima ya afya NHIF 2024 (Bei na Gharama Zake) Kwenye makala hii tutachambua kwa kina gharama na bei za kulipia ili kupata aina fulani ya vifurushi vya bima ya afya kutoka NHIF Pia utapata mchanganuo wa Vifurushi vipya vifurushi vya bima ya afya.

Katika jitihada za kuboresha upatikanaji wa huduma za afya nchini, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umeanzisha vifurushi vipya vya bima ya afya kwa mwaka 2024. Uzinduzi wa vifurushi hivi utafanywa rasmi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu, katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Hii ni hatua muhimu inayolenga kuwafikia wananchi wa makundi mbalimbali kulingana na mahitaji yao ya matibabu.

Huduma Zitakazotolewa na Vifurushi

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, vifurushi hivi vimebuniwa kumwezesha kila Mtanzania kujiunga na bima ya afya kwa kuzingatia uwezo wake kifedha na mahitaji binafsi. Huduma hizi zitatolewa kwa mtu mmoja, mtu na mwenza wake, mtu na mtoto au watoto, na hata familia nzima. Mfumo huu unalenga kupunguza mzigo wa gharama za matibabu kwa wananchi wengi zaidi.

Kabla ya uzinduzi, kampeni kubwa ya usajili wa wananchi itafanyika kwa lengo la kuelimisha na kuwahamasisha watu kujiunga na bima hizi. Pia, kutakuwa na huduma za bure za kupima afya kwa wananchi wote, huduma hizi zitaanza Novemba 25 katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni.

Bei na Gharama za Vifurushi

Katika vifurushi hivi, bei imegawanywa kulingana na umri wa mwanachama na idadi ya watu ndani ya kifurushi. Kwa mtu mmoja mwenye umri wa miaka 18 hadi 35, vifurushi ni kama ifuatavyo:

Umri (Miaka) Kifurushi Bei (TSh)
18 – 35 Najali Afya Premium 192,000
Wekeza Afya 384,000
Timiza Afya 516,000
36 – 59 Najali Afya Premium 240,000
Wekeza Afya 444,000
Timiza Afya 612,000
60+ Najali Afya Premium 360,000
Wekeza Afya 660,000
Timiza Afya 984,000

Gharama ya vifurushi hivyo inaongezeka kwa familia kulingana na idadi ya watu wanaounganishwa, mfano mtu binafsi na watoto wanne kwa umri wa miaka 18 hadi 35:

Kifurushi Bei (TSh)
Najali Afya Premium 636,000
Wekeza Afya 1,092,000
Timiza Afya 1,548,000

Kwa familia yenye watoto wanne na umri wa miaka 36 hadi 59, gharama ya vifurushi vya Timiza Afya ni Sh1,644,000.

Kauli ya Rais Samia Suluhu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu, alitoa hotuba akisisitiza kwamba serikali imeweka mikakati thabiti ya kuimarisha sekta ya afya nchini. Kwa mujibu wa hotuba yake, serikali imewekeza sana katika miundombinu ya afya ili kuhakikisha huduma bora zinapatikana kwa wote.

“Serikali ina mpango wa kuanzisha bima ya afya kwa wananchi wote ili kumudu gharama za matibabu. Tayari tumeshajenga vituo vipya vya afya 352 na hospitali 67 za wilaya pamoja na hospitali 6 za mikoa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya,” alisema Rais Samia.

NHIF imeleta suluhisho bora kwa changamoto ya gharama za matibabu nchini kupitia vifurushi hivi vya bima ya afya. Kila mmoja ana nafasi ya kuchagua kifurushi kinachomfaa kulingana na uwezo wake na mahitaji yake. Serikali kupitia mifumo ya afya inahakikisha huduma bora na nafuu zinawafikia wananchi wote ili kufanikisha lengo la afya kwa wote.